Monday 23 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

LIGI KUU ENGLAND: Leo ni Man City v Liverpool
Vigogo wawili wa Ligi Kuu leo wanakwaana Uwanja wa City of Manchester hili likiwa pambano la tatu mfululizo kwa Vigogo kuvaana.
Wiki iliyokwisha Tottenham na Manchester City zilikutana katika mechi zao za kwanza za Ligi Kuu na kutoka sare 0-0 na pia Liverpool iliivaa Arsenal na kutoka sare 1-1.
Leo ni Man City na Liverpool.
Man City, wakitumia musuli yao ya kifedha, wamelundika Wachezaji wapya Msimu huu ambao ni David Silva, Aleksandr Kolarov na Yaya Toure ambao wote walicheza mechi na Tottenham lakini kwa leo wanaweza wakaongezeka Wachezaji wapya wengine James Milner na Mario Balotelli na wale wa zamani kina Jo na Robinho ambao walikuwa nje kwa mkopo Msimu uliopita.
Kwa Meneja wa Man City, Roberto Mancini, ugumu ni kupanga Timu hasa ukizingatia lundo la Wachezaji hao Mastaa na nini utakuwa uamuzi wake wa nani kucheza Kiungo kati ya Yaya Toure, Nigel de Jong, Gareth Barry na Patrick Viera, unangojewa kwa hamu na wadau.
Msimu uliokwisha, Timu hizi zilitoka sare katika mechi zao mbili za Ligi Kuu.
Liverpool wataingia Uwanjani bila ya mchezaji mpya Joe Cole ambae aliwashwa Kadi Nyekundu katika mechi ya Wikiendi iliyopita dhidi ya Arsenal na hivyo sasa anatumikia kifungo cha mechi tatu baada ya kuamua kutokata rufaa.
Lakini Mchezaji wao mpya mwingine, Christian Poulsen, kuenda akawemo dimbani kwenye Kiungo pamoja na Javier Mascherano ambae amepona maumivu yaliyomfanya atolewe kwenye mechi na Arsenal.
Vikosi vinategemewa kuwa:
Man City: Hart, Bridge, K.Toure, Kompany, Richards, Barry, Yaya Toure, De Jong, Milner, Silva, Tevez.
Liverpool: Reina, Aurelio, Carragher, Skrtel, Johnson, Poulsen, Mascherano, Kuyt, Jovanovic, Gerrard, Torres.

No comments:

Powered By Blogger