Tuesday 24 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

MSIMU MPYA WA UEFA ULAYA KUPAMBWA WIKI HII!!!
Ingawa mechi za Mtoano na Mchujo za Makombe ya UEFA CHAMPIONS LIGI na EUROPA LIGI zimekuwa zikindirima ili kuzipata Timu zitakazoingia Droo ya Makundi ya Mashindano hayo, UEFA watazindua rasmi Msimu wao mpya wa 2010/11 huko Monaco wiki hii kwa kutangazwa kwa Wachezaji Bora wa Ulaya wa Mwaka, kugombewa kwa kwa Kombe la UEFA SUPERCUP kati ya Bingwa wa UEFA CHAMPIONS LIGI, Inter Milan, na Club Atletico de Madrid, Bingwa wa EUROPA LIGI, hapo Alhamisi, na pia kufanyika Droo ya Makundi kwa Mashindano ya Ulaya.
Ratiba ya UEFA inaonyesha Tuzo za Wachezaji Bora zitafanyika Alhamisi Agosti 26 pamoja na Droo ya kupanga Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI huku Mechi za Makundi hayo kuanza kuchezwa Septemba 14 na 15.
Droo ya Makundi ya EUROPA LIGI itafanyika Ijumaa Agosti 27 na kufuatiwa na pambano la kugombea UEFA SUPERCUP kati ya Inter Milan na Atletico Madrid Uwanjani Stade Loius II.
LEO NA KESHO NI SOKOMOKO ULAYA!!
• Timu kugombea Dola Milioni 19!!!!
Jumanne, Agosti 24
UEFA CHAMPIONS LIGI: Hatua ya Mchujo kuingia Makundi-Mechi za Marudiano
Anderlecht v Partizan Belgrade, (Mechi ya kwanza 2-2)
FC Sheriff Tiraspol v Basle, (0-1)
Hapoel Tel-Aviv v Red Bull Salzburg, (3-2)
Sampdoria v Werder Bremen, (1-3)
Sevilla v Braga, (0-1)
EUROPA LIGI: Hatua ya Mchujo kuingia Makundi-Mechi ya Marudiano
Anorthosis Famagusta v CSKA Moscow, (0-4)
Jumatano, 25 Agosti 2010
UEFA CHAMPIONS LIGI:Hatua ya Mchujo kuingia Makundi-Mechi za Marudiano
Ajax v Dynamo Kiev, (Mechi ya kwanza 1-1)
Auxerre v Zenit St Petersburg, (0-1)
FC Copenhagen v Rosenborg, (1-2)
MSK Zilina v Sparta Prague, (2-0)
Tottenham v Young Boys, (2-3)
Timu zinazocheza hatua ya Makundi kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI huwa na uhakika wa kupata angalau Dola Milioni 19 kila moja na leo na kesho Timu 20 zipo kwenye kinyang’anyiro cha Mechi za Marudiano za Hatua ya Mchujo ili kupata Timu 10 ambazo Alhamisi Agosti 26 jioni zitaingia kwenye Kapu la Droo ya kupanga Makundi ya Mashindano hayo wakijumuika na Timu Mabingwa, kama vile Inter Milan, Real Madrid, Manchester United, Barcelona, Arsenal na Chelsea, ambao wameingizwa moja kwa moja Hatua ya Makundi.
Timu hizo 20 zitakazocheza Mechi za Marudiano leo na kesho zilikutana kwenye Mechi ya Kwanza Wiki iliyopita na kati ya hizo ni Timu mbili tu ndizo zimelekea kushika hatamu ya kujihakikishia kuingia Hatua ya Makundi.
Timu hizo ni Zilina ya Slovakia ambayo iliifunga Spart Prague 2-0 ugenini na, pengine, Hapoel Tel Aviv ambayo iliifunga Red Bull Salzburg 3-2 ugenini.
Timu ya Ligi Kuu England, Tottenham, ilicheza ugenini huko Uswisi na Young Boys na kujikuta iko nyuma kwa bao 3-0 hadi dakika ya 28 ya mchezo lakini ikajitutumua na kupata matokeo ya 3-2 ambayo yatawapa matumaini makubwa kuwatungua Young Boys watakapowaalika Uwanjani kwao, White Hart Lane, Jijini London hapo kesho.
Pia leo kutakuwa na Mechi moja ya Hatua ya Mchujo ya EUROPA LIGI kati ya Anorthosis Famagusta v CSKA Moscow, (Matokeo Mechi ya kwanza 0-4) na mechi zote nyingine kuchezwa Alhamisi Agosti 26.

No comments:

Powered By Blogger