Sunday 22 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com


Newcastle 6 Aston Villa 0
Wakiwa nyumbani, St James Park, wakicheza mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu tangu wapande Daraja, Newcastle leo imewapa furaha kubwa baada ya kuinyuka Timu ngumu Aston Villa bao 6-0.
Wakati mechi iko 0-0, John Carew aliikosesha Villa bao pale penalti yake ilipoota mbawa.
Hadi mapumziko Newcastle walikuwa mbele kwa bao 3-0 zilizofungwa na Viungo Joey Barton na Kevin Nolan, na la tatu na Straika Andy Carroll.
Kipindi cha pili, Carroll akafunga bao mbili na Kevin Nolan akapata bao lake la pili na la 6 kwa Newcastle.
Vikosi vilivyoanza:
Newcastle: Harper, Perch, Coloccini, Williamson, Jose Enrique, Routledge, Smith, Barton, Gutierrez, Nolan, Carroll.
Akiba: Krul, Lovenkrands, Ryan Taylor, Xisco, Ameobi, Vuckic, Tavernier.
Aston Villa: Friedel, Luke Young, Clark, Dunne, Warnock, Albrighton, Petrov, Ireland, Downing, Ashley Young, Carew.
Akiba: Guzan, Delfouneso, Heskey, Reo-Coker, Beye, Lichaj, Bannan.
Refa: Martin Atkinson
Scholes kudumu Man United
Paul Scholes amesema ataendelea kucheza Manchester United kwa muda mrefu zaidi ikiwa Klabu itamuona bado anahitajika.
Scholes, Miaka 35, anatimiza Miaka 18 akiwa yupo Manchester United na ameanza Msimu huu mpya kwa kung’ara sana hasa katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu walipoifunga Newcastle bao 3-0 na yeye kuwa ndio Mchezaji Bora wa Mechi hiyo.
Scholes ametamka: “Nimebaki hapa kwani ni Klabu Bora! Mie Mzawa wa Manchester sina sababu kuondoka. Meneja akiendelea kunihitaji, ntaendelea kucheza. Huwezi kuchoshwa na kushinda Vikombe! Huchoki kushinda kila wiki! Nani atachoka hilo?”
Lyon wamwania Robinho
Lyon ya Ufaransa imeingia kwenye mbio za kutaka kumchukua Robinho ambae amekuwa hataki kubaki Manchester City baada ya kumaliza Mkataba wa mkopo na Klabu ya kwao Brazil Santos.
Inasadikiwa Man City washanyosha mikono kwa Robinho na sasa wana nia tu ya kujaribu kurudisha Pauni Milioni 32.5 walizomnunulia Septemba 2008.
Ingawa Robinho yumo mwenye Kikosi cha Man City walichokisajili kwa ajili ya EUROPA LIGI hakuwemo kwenye mechi na FC Timisoara Alhamisi iliyopita kwa vile Man City hawataki kutibua soko lake kwani akiichezea Man City kwenye mashindano hayo hataruhusiwa kuichezea Klabu nyingine Ulaya Msimu huu.
Inasemekana Lyon wametoa ofa ya kumchukua Robinho kwa mkopo lakini Man City wanataka kumuuza moja kwa moja.

No comments:

Powered By Blogger