Thursday 26 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

UEFA CHAMPIONS LIGI: Droo ya Makundi leo!!!
Washindi 10 wa Hatua ya Mchujo wameshapatikana kwa matokeo ya Mechi za jana Jumatano na juzi Jumanne na wataungana na Timu 22 Vigogo ambao wameingizwa moja kwa moja katika Hatua ya Makundi ili kupangwa Makundi manane ya Timu nne nne kila Kundi katika Droo itakayofanyika leo jioni.
Mechi za Makundi zitachezwa kuanzia Septemba hadi Desemba na washindi wawili wa kila Kundi watasonga Hatua ya Kwanza ya Mtoano.
Timu zitakazoshika nafasi ya tatu katika Makundi zitatupwa kwenye EUROPA LIGI Hatua ya Mtoano ya Timu 32.
TIMU 32 ZA KWENYE DROO:
ZILIZOINGIA MOJA KWA MOJA:
-Arsenal
-Barcelona
-Bayern Munich
-Benfica
-Bursaspor
-CFR Cluj
-Chelsea
-Inter Milan
-Lyon
-Man United
-Marseille
-AC Milan
-Panathinaikos
-Rangers
-Real Madrid
-AS Roma
-Rubin Kazan
-Schalke
-Shakhtar Donetsk
-Spartak Moscow
-FC Twente
-Valencia
TIMU 10 TOKA MCHUJO:
-Partizan Belgrade
-Basle
-Hapoel Tel-Aviv
-Werder Bremen
-Braga
-Tottenham
-Ajax Amsterdam
-Auxerre
-FC Copenhagen
-MSK Zilina

No comments:

Powered By Blogger