Wednesday 25 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Bongo yapepea Ligi Kuu England!!
Bodi ya Utalii Tanzania, TTB, imesema Wizara ya Maliasili na Utalii ikishirikiana na Mamlaka zake tanzu TTB, TANAPA [Mamlaka ya Hifadhi za Wanyama] na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, zimeingia Mkataba na Lantech Service Agency ya Uingereza ili kutoa matangazo kwenye Mechi 114 za Ligi Kuu England kwa Msimu wa 2010/11.
Matangazo hayo yanayohusu Mbuga za Wanyama, Mlima Kilimanjaro na Bichi za Zanzibar yatakuwa yakionyeshwa wakati wa Mechi kwenye Matangazo ya Dijito yaliyo pembezoni na yanayozunguka Uwanja mzima katika Viwanja vya Timu 6 za Ligi Kuu.
Viwanja hivyo ni Ewood Park, Uwanja wa Blackburn Rovers, St James Park, Uwanja wa Newcastle, Stadium of Light wa Sunderland, Molineux wa Wolves, Britannia wa Stoke City na The Hawthorns wa West Bromwich Albion.
Matangazo hayo yatadumu sekunde 30 kwenye bodi za Matangazo kuzunguka Viwanja hivyo na yataonekana mara 6 kila Mechi.
Matangazo hayo yalianza kuonekana kwa mara ya kwanza kwenye Mechi za Blackburn v Everton, Sunderland v Birmingham and Wolves v Stoke City hapo Agosti 14.
Robinho aigomea Fenerbahce
Fowadi wa Manchester City Robinho amekataa kuhamia Klabu ya Uturuki Fenerbahce na ameng’ang’ania kuhamia Italy au Spain kabla ya Jumanne ijayo Agosti 31 ambayo ndio Siku ya mwisho kwa uhamisho.
Robinho amelazimika kurudi Manchester City baada ya kukaa huko kwao Brazil na Klabu ya Santos kwa mkopo wa Miezi 6.
Robinho alisajiliwa kwa pauni Milioni 32.5 Mwaka 2008 ikiwa ni rekodi kwa Uingereza akitokea Real Madrid lakini amekuwa hapataki Man City.
Man City imewagomea Santos kuongeza mkopo wake na badala yake wanataka kumuuza moja kwa moja ili warudishe fedha zao.
Ingawa Meneja wa Man City, Roberto Mancini, amekiri Robinho anataka kuondoka, yeye ameacha milango wazi kwake kwa kusema ikiwa atafanya mazoezi kwa bidii anaweza kucheza Man City.
Fergie aiunga mkono England Kombe la Dunia 2018
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson ameyapa uzito maombi ya England kuwa Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia la Mwaka 2018 kwa kuipamba England kabla hajakutana na Wakaguzi wa FIFA ambao wako England kwa ziara ya Siku 4 kukagua Maombi hayo pamoja na Viwanja mbalimbali, ukiwemo Old Trafford ambako Sir Alex Ferguson na Sir Bobby Charlton watawakaribisha Wakaguzi hao 6 wa FIFA.
Ferguson, akitoa sapoti yake kwa England, alitamka: “Viwanja kwa Wachezaji na Mashabiki ni vizuri sana! Na mapenzi ya Waingereza kwa Soka yatahakikisha kila Mtu anakaribishwa na kupata wakati mzuri.”

No comments:

Powered By Blogger