Tuesday 24 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Man City waifumua Liverpool 3-0
Goli mbili toka kwa Carlos Tevez na moja la Gareth Barry zilishusha kipondo cha 3-0 toka Kwa Manchester City dhidi ya Liverpool Uwanjani City of Manchester mbele ya Watazamaji 47,087 mmoja wao akiwa Mmiliki Tajiri wa Man City Sheikh Mansour ambae ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufika Uwanjani hapo.
Klabu Tajiri kwenye Ligi Kuu, Man City, iliyotumia zaidi ya Pauni Milioni 125 kununua Wachezaji Msimu huu, ilifunga bao la kwanza toka kwa Gareth Barry dakika ya 13 na hadi mapumziko matokeo yalikuwa 1-0.
Kipindi cha pili Carlos Tevez alipachika bao mbili, dakika ya 52 na 67.
Liverpool, wakitumia mfumo wa 4-4-2 bila ya Kiungo nanga Javier Mascherano ambae habari zimepamba moto kuwa mguu nje kwenda FC Barcelona, walizidiwa musuli kila idara huku Man City ikitawala kiungo kupitia Wachezaji wao Yaya Toure, Gareth Barry, Nigel de Jong, wakisaidiwa na James Milner na Winga Adam Johnson.
Vikosi vilivyoanza:
Manchester City (4-3-3): Hart; Richards, Kolo Toure, Kompany, Lescott; Yaya Toure, De Jong, Barry; Johnson, Tevez, Milner.
Akiba: Given, Zabaleta, Wright-Phillips, Adebayor, Silva, Vieira, Jo.
Liverpool (4-4-2): Reina; Johnson, Skrtel, Carragher, Agger; Jovanovic, Gerrard, Lucas, Kuyt; Torres, Ngog.
Akiba: Jones, Aurelio, Pacheco, Kyrgiakos, Maxi, Babel, Poulsen.
Refa: Phil Dowd

No comments:

Powered By Blogger