Wednesday 25 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Tottenham wawabonda Young Boys 4-0
Kwa mara ya kwanza tangu 1961, Tottenham wamefuzu kuingia Mashindano makubwa ya Ulaya walipowabonda Young Boys ya Uswisi kwa mabao 4-0 Uwanjani White Hart Lane kwenye mechi ya marudiano Hatua ya Mchujo kuingia kwenye Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Kwenye mechi ya kwanza huko Uswisi, Tottenham walichapwa kwa bao 3-2 hivyo wamefuzu kwa jumla ya mabao 6-3.
Mabao ya Tottenham yalifungwa na defoe, dakika ya 5 na Peter Crouch mabao matatu, dakika ya 32, 61 na 77 kwa penalti.
Droo ya kugawa Makundi itafanyika Alhamisi Agosti 26.
MATOKEO KAMILI:
UEFA CHAMPIONS LIGI: Hatua ya Mchujo kuingia Makundi-Mechi za Marudiano
Jumatano, 25 Agosti 2010
Ajax 2 v Dynamo Kiev 1, (Mechi ya kwanza 3-2)
Auxerre 2 v Zenit St Petersburg 0, (2-1)
FC Copenhagen 1 v Rosenborg 0, (2-2, FC Copenhagen yapeta goli la ugenini)
MSK Zilina 1 v Sparta Prague 0, (3-0)
Tottenham 4 v Young Boys 0, (6-3)

No comments:

Powered By Blogger