Friday 27 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

UEFA SUPERCUP: Inter Milan v Atletico Madrid
Leo huko Monaco, ndani ya Stade Louis II, Msimu mpya wa Ulaya wa 2010/11 utaanuliwa rasmi kwa pambano la kugombea UEFA SUPERCUP kati ya Mabingwa wa UEFA CHAMPIONS LIGI, Inter Milan ya Italia na Atletico Madrid ya Spain, ambao ndio Mabingwa wa EUROPA LIGI.
Mechi hii, itakayoanza Saa 3 dakika 45 usiku, saa za bongo, itakuwa chini ya usimamizi wa Refa Massimo Busacca wa Uswisi.

No comments:

Powered By Blogger