Saturday 28 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

UEFA SUPERCUP: Atletico watwaa Kombe!
• Atletico 2 Inter Milan 0
Jana usiku huko Monaco, Mabingwa wa EUROPA LIGI, Atletico Madrid, wametwaa UEFA Supercup kwa kuwafunga Mabingwa wa UEFA CHAMPIONS LIGI, Inter Milan, mabao 2-0.
Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Jose Antonio Reyes, ndie aliefunga bao la kwanza kwenye dakika ya 62 na dakika ya 83 Sergio Aguero akapachika bao la pili.
Mchezaji Bora Ulaya, Diego Milito, alikosa penalti dakika ya 90.
Msimu uliokwisha, Inter Milan chini ya Kocha Jose Mourinho ambae sasa yuko Real Madrid, walitwaa Ubingwa wa Italia, Kombe la Italia na UEFA CHAMPIONS LIGI.
Msimu huu Inter Milan wako chini ya Kocha wa zamani wa Liverpool, Rafael Benitez, na wiki iliyopita walitwaa Italian Supercup kwa kuifunga AS Roma 3-1.
BUNDESLIGA: FC Kaiserslautern 2 Bayern Munich 0
Hapo jana, kwenye mechi ya Ligi ya Bundesliga huko Ujerumani, FC Kaiserslautern iliwafunga Mabingwa Bayern Munich kwa bao 2-0.
Mabao ya dakika ya 36 na 37 ya Ivo Ilicevic na Srdjan Lakic ndio yaliowatoa nishai Mabingwa hao.
Mechi zingine za Bundesliga zitachezwa leo na kesho.

No comments:

Powered By Blogger