Tuesday 24 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Evra kukatia Rufaa kifungo!
Patrice Evra ameamua kukata Rufaa kupinga adhabu ya kufungiwa Mechi 5 za Timu ya Taifa ya Ufaransa kwa ushiriki wake katika mgomo wa Wachezaji wa Ufaransa huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia.
Evra ndie alikuwa Nahodha wa Ufaransa huko Afrika Kusini na mgomo wa Wachezaji ulitokea baada ya mwenzao Nicolas Anelka kufukuzwa kwenye Timu baada ya kugombana na aliekuwa Kocha wa Ufaransa Raymond Domenech.
Pamoja na Evra, Wachezaji wengine waliofungiwa ni Anelka, mechi 18, Franck Ribery, mechi 3 na Jeremy Toulalan, mechi moja.
Kocha mpya wa Ufaransa, Laurent Blanc, ambae tayari aliwaadhibu Wachezaji wote 23 waliokuwa Afrika Kusini kwa kutowaita kwenye mechi ya kirafiki na Norway mwanzoni mwa Mwezi huu, ameshangazwa na ukali wa adhabu zilizotolewa pamoja na kutofautiana kwa urefu wake kwa kosa ambalo aliliita ni moja na la Wachezaji wote kwa pamoja.
‘Mtu Spesheli’ anena: ‘Ni Chelsea, Man United na Man City! Ze Gunners na Liverpool hawana lao!’
Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho ametamka kuwa Arsenal na Liverpool hawana chao Msimu huu kwa kuwa hawana ubavu wa kutwaa Ubingwa.
Mourinho, maarufu kama ‘Mtu Spesheli’, ambae aliwahi kuwa na Chelsea kwa Miaka mitatu, ametabiri kuwa vita ya Ubingwa ni ya Chelsea, Manchester United na Manchester City.
Mourinho alitamka: ‘Naamini ni Chelsea, Manchester United na Manchester City ndizo Timu zinaweza kuwa Bingwa. Ni ngumu kumuona Roy Hodgson akileta mafanikio Liverpool ambayo imezidi kuwa mbovu Mwaka hadi Mwaka. Liverpool ya 2004 ilikuwa bora kupita ya 2005! Ile ya 2005 ilikuwa bora kupita ya 2006 na kadhalika!”
Kuhusu Arsenal, Mourinho ametoa mawazo yake kuwa Meneja wao, Arsene Wenger, siku zote amekuwa akitoa kisingizio Kikosi chake ni kichanga.
Mourinho alieleza: “Kila Mwaka Arsenal huonekana wanakaribia Ubingwa lakini hamna kitu! Siku zote wanasema ni Timu changa, mwakani itakuwa bora! Lakini Timu ya Chipukizi ya jana si leo tena ni chipukizi! Sasa wamefika Miaka 25, 26 na 27 na ni lazima washinde! Fabregas, Walcott, Clichy, Song na Sagna si watoto tena! Wako kwenye umri wa kuwa Mabingwa! Lakini sidhani kama wana uwezo, nadhani ni Chelsea au Manchester United na Manchester City ambao wana Kikosi kizuri!”

No comments:

Powered By Blogger