Saturday 28 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

LIGI KUU: Chelsea yashinda tena, Spurs yatunguliwa kwao!
MATOKEO: Mechi za leo Jumamosi Agosti 28
Blackburn 1 v Arsenal 2
Blackpool 2 v Fulham 2
Chelsea 2 v Stoke 0
Tottenham 0 v Wigan 1
Wolverhampton 1 v Newcastle 1
Baada ya kuchapwa jumla ya mabao 10 katika mechi mbili za kwanza za Ligi Kuu walizocheza kwao Uwanja wa DW, leo Wigan walisafiri hadi Jijini London kucheza na Tottenham katika Uwanja wa White Hart Lane ambao Msimu uliokwisha Wigan walikung’utwa mabao 9-1 lakini leo Straika Hugo Rodallega alliwapa furaha kubwa kwa kufunga bao moja na la ushindi kwenye dakika ya 80.
Mabingwa Chelsea leo wameshinda ila wameshindwa kutoa dozi ya mabao 6 kama walivyofanya katika mechi zao mbili za kwanza na badala yake wameshinda 2-0 kwa mabao ya Malouda na Drogba, aliefunga kwa penalty.
Awali, Lampard alikosa penalti baada ya Kipa Sorensen kuicheza.
Mechi nyingine mbili zilimalizika kwa sare ambapo Wolves na Newcastle iliisha 1-1 na Blackpool v Fulham 2-2.

No comments:

Powered By Blogger