Saturday 28 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Man United 3 West Ham 0
Wakiwa nyumbani Old Trafford, Manchester United wameifunga West Ham mabao 3-0 kwenye Mechi ya Ligi Kuu.
Hiki ni kipigo cha tatu mfululizo kwa West Ham na wamefungwa Mechi zote za Ligi Kuu tangu Msimu huu uanze.
Man United walipata bao la kwanza dakika ya 34 baada ya Giggs kuchanja mbuga ndani ya boksi na kuangushwa na Jonathan Spector, Mchezaji wa zamani wa Man United, na Refa Clattenburg akatoa penalti iliyofungwa na Rooney ambalo hilo ni goli lake la kwanza tangu Mwezi Machi.
Licha ya kutawala, hadi mapumziko Man United walikuwa mbele 1-0.
Kipindi cha Pili muvu nzuri kati ya Scholes na Rooney ilitua kwa Nani aliehadaa Mabeki ndani ya boksi na kufunga bao dakika ya 49.
Berbatov aliunganisha krosi ya Nani na kupachika bao la 3 dakika ya 69.
Vikosi vilivyoanza:
Man United: Van der Sar, O'Shea, Vidic, Jonathan Evans, Evra, Nani, Scholes, Fletcher, Giggs, Rooney, Berbatov.
Akiba: Kuszczak, Owen, Smalling, Hernandez, Carrick, Rafael Da Silva, Valencia.
West Ham: Green, Spector, Gabbidon, Upson, Ilunga, Faubert, Noble, Parker, Boa Morte, Dyer, Cole.
Akiba: Stech, Barrera, Kovac, McCarthy, da Costa, Stanislas, Piquionne.
Refa: Mark Clattenburg

No comments:

Powered By Blogger