Friday 27 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

EUROPA LIGI: Villa nje, Liverpool & Man City zapeta!
  •  Celtic yabwagwa!
Aston Villa, ikiwa kwao Villa Park, ilichapwa 3-2 na Rapid Vienna na kubwagwa nje ya EUROPA LIGI baada ya kutoka sare 1-1 mechi ya kwanza.
Wenzao wa Ligi Kuu Liverpool na Manchester City walishinda mechi zao za marudiano na kujihakikishia leo kuwemo kwenye Droo ya kupanga Makundi ya EUROPA LIGI.
Man City, wakicheza nyumbani City of Manchester Stadium, waliichapa FC Timisoara 2-0 na hivyo kuwatoa nje Timu hiyo ya Roumania kwa jumla ya mabao 3-0 baada ya kushinda mechi ya kwanza ugenini kwa bao 1-0.
Mabao ya Man City yalifungwa Kipindi cha Pili na Shaun Wright-Phillips na Boyata.
Liverpool, wakicheza ugenini huko Uturuki, walijikuta wako nyuma dakika ya 3 tu, lakini walikaza mshipi na kufunga bao mbili kupitia Kacar, aliejifunga mwenyewe, dakika ya 84 na Kuyt dakika ya 88.
Nayo, Timu kongwe ya Scotland, Celtic, imebwagwa nje ya EUROPA LIGI na FC Utrecht ya Uholanzi baada ya kuchapwa 4-0 kwenye mechi ya marudiano.
Celtic ilishinda mechi ya kwanza 2-0.

No comments:

Powered By Blogger