Wednesday 25 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

‘Mtu Spesheli’ anena: ‘England itashindwa chini ya Capello!’
• Mourinho aifutia mafanikio chini ya Mtaliana huyo!
Jose Mourinho amedai England haiwezi kufanikiwa ikiwa chini ya Kocha kutoka Italia Fabio Capello kwa vile hana uhusiano mzuri na Wachezaji wake.
Huko England, Magazeti mengi, hasa yale ya Mitaani, yameanza wimbi la kumponda Capello huku moja likimwita Capello ‘punda’.
Mourinho, ambae jana aliwakandya Rafael Benitez, Arsene Wenger na Liverpool, ametamka: “Tatizo ni Capello, Capello hawezi kuifanikisha England!”
Capello aliwahi kuwa Kocha wa Real Madrid ambayo ndiyo Klabu ya sasa ya Mourinho na ‘Mtu Spesheli’ amesema: “Muulize yeyote hapa Real na watakwambia Capello hawezi kubadilika! Huwezi kuwapigia kelele Wachezaji wako! Wachezaji hao wanataka waonekane ni Watu spesheli!”
Mourinho akaongeza: “Ni wazi Capello hataisaidia England. Hawajui Wachezaji na Wachezaji wanamwogopa. Ni vurugu tu! Wachezaji wanahitaji mbinu za wazi na si kuchanganywa. Ni tatizo la Meneja. Ni aibu hii!”
Minong’ono: Man United kumnasa Defour kabla Dirisha kufungwa!
Kuna taarifa nzito zimeibuka kuwa Manchester United huenda wakamchota Kiungo anaesifika kutoka Standard Liege ya Ubelgiji, Steven Defour, ambae amekuwa kwenye rada za Klabu hiyo kwa muda mrefu kabla Dirisha la uhamisho halijafungwa hapo Agosti 31.
Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, aliwahi kumtumia barua Mchezaji huyo hapo Mwaka jana kumpa pole na kumtakia apone haraka baada ya kuumia vibaya mguu wake.
Wakati Klabu kadhaa za Ulaya zikimkodolea macho kuna dalili Man United itamnyakua Defour, ambae ni Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Ubelgiji, ili kuziba pengo la Owen Hargreaves ambae kurudi kwake Uwanjani ni kitendawili baada ya magoti yake kushindwa kutengemaa.

No comments:

Powered By Blogger