Sunday 22 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Fulham 2 Man United 2
Leo uwanjani Craven Cottage, Fulham wameweza kuisimamisha Manchester United na kutoka nao sare 2-2 katika mchezo mkali wa vuta nikuvute.
Pengine matokeo hayo ni mazuri kwa Man United hasa ukichukulia katika Misimu miwili iliyopita wamekuwa wakifungwa Uwanjani hapo.
Man United ndio waliopata bao kwanza dakika ya 11 Mfungaji akiwa Mkongwe Paul Scholes.
Kipindi cha Pili Simon Davies alisawazisha dakika ya 57.
Beki wa Fulham Brede Hangeland alijifunga mwenyewe kwenye dakika ya 84 na kuwapa Man United bao la pili.
Kwenye dakika ya 85, Nani aliikosesha Man United ushindi pale aliposhindwa kufunga penalti iliyookolewa na Kipa Stockdale.
Ndipo kwenye dakika ya 89 Hangeland akafuta makosa yake alipofunga bao la kichwa kufuatia kona na kufanya mechi iwe 2-2.
Vikosi vilivyoanza:
Fulham: Stockdale, Pantsil, Hughes, Hangeland, Konchesky, Duff, Murphy, Etuhu, Davies, Dempsey, Zamora.
Akiba: Zuberbuhler, Kelly, Baird, Gera, Riise, Greening, Dembele.
Man Utd: Van der Sar, O'Shea, Vidic, Jonathan Evans, Evra, Valencia, Fletcher, Scholes, Park, Hernandez, Berbatov.
Akiba: Kuszczak, Owen, Giggs, Smalling, Carrick, Nani, Rafael Da Silva.
Refa: Peter Walton

No comments:

Powered By Blogger