Friday 27 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

LIGI KUU ENGLAND: Tathmini Mechi za Wikiendi hii
Jumamosi, 28 Agosti 2010
[saa za bongo]
[saa 8 dak 45 mchana]
Blackburn v Arsenal
[saa 11 jioni]
Blackpool v Fulham
Chelsea v Stoke
Tottenham v Wigan
Wolverhampton v Newcastle
[saa 1 na nusu usiku]
Man Utd v West Ham
Jumapili, 29 Agosti 2010
[saa 9 na nusu mchana]
Bolton v Birmingham
[saa 11 jioni]
Liverpool v West Brom
Sunderland v Man City
[saa 12 jioni]
Aston Villa v Everton
Timu zote 20 za Ligi Kuu zitajimwaga dimbani kucheza Mechi zao za tatu za Ligi hapo kesho na Jumapili.
Mechi ya kwanza ya Wikiendi ni ile ya Saa 8 dakika 45 mchana Jumamosi huko Ewood Park kati ya Wenyeji Blackburn Rovers na Arsenal.
Msimu uliokwisha, Blackburn ilishinda 2-1 na kumfanya Arsene Wenger alalamike mibavu ya Blackburn ambao wamefungwa mechi moja tu kati ya 11 za mwisho za Ligi Kuu kuchezewa Uwanjani kwao.
Tayari Wenger ashaanza kuigwaya mechi hii kwa kumtaka Refa aidhibiti vizuri.
Wigan, baada ya kutandikwa jumla ya mabao 10 kati mechi zao mbili za kwanza za ligi Msimu huu, wanasafiri hadi Jijini London, Uwanjani White Hart Lane, nyumbani kwa Tottenham ambao waliinyuka Wigan mabao 9-1 Msimu uliopita.
Chelsea ndio Timu pekee Msimu huu iliyoshinda mechi zake mbili ilizocheza kwa mabao 6-0 kila moja na kesho wanawakaribisha Stoke City huko Stamford Bridge ambao Msimu uliokwisha walipigwa 7-0 Uwanjani hapo.
Baada ya Meneja wao, Sir Alex Ferguson, kukiri sare ya 2-2 na Fulham huko Craven Cottage wiki iliyopita ilikuwa ni kupoteza pointi kipumbavu, kesho Manchester United wataivaa West Ham, Timu ambayo imepoteza mechi zake zote mbili za Ligi, Uwanjani Old Trafford.
Baada ya kuiwasha Aston Villa 6-0, Newcastle inaenda kucheza na Wolves ambayo, baada ya mechi mbili, imeshinda mechi moja na kutoka sare mechi moja Msimu huu.
Blackpool,Timu iliyopanda Daraja Msimu huu, ilishinda mechi ya kwanza kwa kuichapa Wigan 4-0 lakini ikapewa somo pale ilipopigwa 6-0 na Arsenal, na wikiendi hii wanacheza mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu Uwanjani kwao dhidi ya Fulham.
Huko Reebok Stadium, Siku ya Jumapili, Bolton wanaikaribisha Birmingham City na hii ni mechi kali ukizingatia viwango vinavyofanana vya Timu hizi.
Liverpool, baada ya kupigwa 3-0 na Manchester City, watakuwa nyumbani kucheza na West Bromwich Albion.
Nao wababe wa Liverpool, Timu Tajiri, Manchester City, wanasafiri kwenda kucheza na Sunderland ambao wametoka sare mechi moja na kufungwa moja.
Mechi ya mwisho ya Wikiendi hii itakuwa huko Villa Park kati ya Aston Villa na Everton.

No comments:

Powered By Blogger