Tuesday 17 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

KIFUNGO: Anelka, mechi 18; Evra, mechi 5 & Ribery,  3!!!!!!
Kamati ya Nidhamu ya FFF, Chama cha Soka France, leo imeamua kuwapa adhabu Wachezaji wanne kati ya watano waliofikishwa mbele yao kujibu tuhuma za kuongoza mgomo wa Wachezaji huko Afrika Kusini kufuatia kufukuzwa kwa Nicolas Anelka baada ya kugombana na Kocha Raymond Domenech.
Anelka amepewa kifungo cha mechi 18 kutoichezea France na Evra amefungiwa mechi 5.
Ribery amepewa adhabu ya mechi 3 na Jeremy Toulalan mechi moja.
Eric Abidal amenusurika adhabu.
Ozil aenda Real
Real Madrid imemnyakua Kiungo wa Ujerumani, Mesut Ozil, alieng’ara na Nchi yake huko Afrika Kusini kwenye Fainali za Kombe la Dunia, kwa ada ya Pauni Milioni 12.4.
Ozit, Miaka 21, anachezea Werder Bremen huko Ujerumani na amebakiza Mwaka mmoja tu kumaliza Mkataba wake hivyo imekuwa ni busara kwa Bremen kumuuza sasa la sivyo Mwakani isingepata hata senti.
Ozit anategemewa kupimwa afya yake hapo kesho Jumatano.

No comments:

Powered By Blogger