Monday 16 August 2010


Fergie aitwa kama Shahidi!!
Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, aliruka hadi Ureno kwenda kumtetea Msaidizi wake wa zamani ambae sasa ni Kocha wa Ureno, Carlos Queiroz, anaepigania kunusuru kibarua chake baada ya kushitakiwa na Chama cha Soka cha Ureno kwa kuwa mkali na kuwatukana Maafisa waliotumwa kuwapima Wachezaji wa Ureno kama wanatumia madawa marufuku au la kabla ya kuanza kwa Fainali za Kombe la Dunia.
Ferguson aliitwa kama shahidi wa upande wa utetezi wa Queiroz ili kuthibitisha tabia nzuri ya Kocha huyo.
Queiroz, ambae alikuwa Msaidizi wa Ferguson kwa Miaka mitano huko Old Trafford, amekana shutuma hizo ambazo akipatikana na hatia nazo huenda akafukuzwa kama Kocha wa Ureno.
Katika utetezi huo, Ferguson alitamka: “Ni Kocha Bora na Mwalimu mzuri na lengo lake maishani ni kuwaendeleza Vijana, kuwapa msukumo na kuhakikisha wanakuwa Watu wema na ndio maana nipo hapa kumtetea kwa vile pia namjua vyema na ni Mtu mwenye utiifu na heshima kubwa! Carlos ni mmoja wa Watu wema!”

No comments:

Powered By Blogger