Thursday 19 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Ze Gunners wamng’ang’ania Schwarzer, Fulham wagomea ofa!
Ofa ya pili ya kumnunua Kipa Veterani wa Fulham, Mark Schwarzer, imekataliwa na Klabu hiyo na Meneja wa Fulham, Mark Hughes, amewataka Arsenal wapandishe dau lao.
Mwezi Mei, Arsenal walitoa ofa ya Pauni Milioni 2 kwa Schwarzer, Miaka 37, na hivi juzi wamerudia tena lakini Fulham wanataka fedha zaidi.
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, yuko sokoni kutafuta Kipa mwingine baada ya Makipa wake, Manuel Almunia na Lukasz Fabiasnky, kuonekana kulegalega, kupwaya na kuwa uchochoro.
Kufuatia kugoma kwa Fulham, taarifa za ndani ya Arsenal zinadai kuwa macho ya Wenger sasa yako kwa Kipa Shay Given wa Manchester City ambae amepigwa benchi na Chipukizi Joe Hart na hivyo kutaka kuhama.
Kipa mwingine mlengwa wa Wenger ni Maarten Stekelenburg wa Ajax ambae pia aliichezea Kombe la Dunia Uholanzi huko Afrika Kusini.

No comments:

Powered By Blogger