Sunday 15 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Liverpool, Arsenal ngoma ngumu 1-1!
• Wachezaji wapya waona Nyekundu!
Ni Bigi Mechi iliyojaa kila aina ya vimbwanga vikiwemo vya Wachezaji wapya wa kila upande kulambwa Kadi Nyekundu katika Mechi yao ya kwanza tu ya Ligi Kuu kutoka kwa Refa Martin Atkinson.
Joe Cole, akiichezea Liverpool mechi yake ya kwanza kwenye Ligi Kuu alipigwa Nyekundu kwa mchezo mbaya dhidi ya Beki mpya wa Arsenal kutoka Ufaransa, Koscielny, kwenye dakika za majeruhi za Kipindi cha kwanza lakini nae Koscielny akatwangwa Nyekundu dakika za lala salama baada ya kupewa Kadi za Njano mbili.
Wakicheza Mtu 10, Liverpool ndio walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 46 kupitia Ngog baada ya pande la Mascherano.
Arsenal walisawazisha bao hilo dakika ya 91 kufuatia kosa la Kipa Reina alieutema wavuni mpira uliogonga mwamba wa Chamakh wa Arsenal baada ya krosi ya Rosicky.
Vikosi vilivyoanza:
Liverpool: Reina, Johnson, Carragher, Agger, Skrtel, Gerrard, Jovanovic, Mascherano, Kuyt, Cole, Ngog.
Akiba: Cavalieri, Aurelio, Torres, Maxi, Babel, Lucas, Kelly.
Arsenal: Almunia, Clichy, Vermaelen, Koscielny, Diaby, Nasri, Eboue, Sagna, Wilshere, Arshavin, Chamakh.
Akiba: Fabianski, Rosicky, van Persie, Vela, Walcott, Song, Gibbs.
Refa: Martin Atkinson

No comments:

Powered By Blogger