Friday 20 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

EUROPA LIGI: Matokeo
• Rapid Vienna 1 v Aston Villa 1
• FC Timisoara 0 v Man City 1
• Liverpool 1 v Trabzonspor 0
Bao la dakika 45 la Ryan Babel limewapa ushindi Liverpool kwa bao 1-0 katika mechi ya kwanza na Trabzonspor ya Uturuki Uwanjani Anfield huku balaa likiendelea kumkumba Mchezaji wao mpya Joe Cole ambae Jumapili alitwangwa Kadi Nyekundu kwenye mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Arsenal na leo akakosa kufunga penalti.
Manchester City wakicheza ugenini huko Romania na Wenyeji wao FC Timisoara waliweza kushinda kwa bao 1-0 Mfungaji akiwa ‘Super Mario’, Bario Balotelli, kwenye dakika ya 72, na hii ikiwa ni mechi yake ya kwanza kwa Klabu yake mpya.
Nao Aston Villa, walitoka sare ugenini na Rapid Vienna kwa bao 1-1.
Marudio ya mechi hizi ni Alhamisi ijayo.

No comments:

Powered By Blogger