Sunday 15 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

MAN UNITED yatangaza Namba za Jezi za Wachezaji
Manchester United imetangaza Namba za Jezi za Wachezaji wake kwa ajili ya Msimu wa 2010/11 wa Ligi Kuu lakini bado haijateua Kikosi chake cha Wachezaji 25 wanaotakiwa kusajiliwa kwa Ligi ili kukidhi Sheria mpya ya kuwa na Wachezaji wa nane kati ya hao 25 ‘waliolelewa’ nyumbani kwa Miaka Mitatu kabla hawajatimiza Umri wa Miaka 21.
‘Kulelewa nyumbani’ kunamaanisha kuwemo kwenye Klabu za England au Wales kwa Miaka mitatu kabla hawajatimiza umri wa Miaka 21.
Man United imesema Kikosi hicho cha Wachezaji 25 kitatangazwa Septemba Mosi ambayo ndio Siku ya mwisho kuwasilisha usajili huo.
Wachezaji wapya, Chris Smalling na Chicharito, wamepewa Jezi Namba 12 kwa Smalling na 14 kwa Chicharito.
Mchezaji mwingine mpya ni Bebe kutoka Ureno lakini bado hajapewa Namba ya Jezi kwa vile usajili wake bado haujakamilika.
Kikosi kamili na Namba za Jezi:
1. Van der Sar, 2. Neville, 3. Evra, 4. Hargreaves, 5. Ferdinand, 6. Brown, 7. Owen, 8. Anderson, 9. Berbatov, 10. Rooney, 11. Giggs, 12. Smalling, 13. Park, 14. Chicharito, 15. Vidic, 16. Carrick, 17. Nani, 18. Scholes, 20. Fabio, 21. Rafael, 22. O'Shea, 23. J Evans, 24. Fletcher, 25. Valencia, 26. Obertan, 27. Macheda, 28. Gibson, 29. Kuszczak, 30. De Laet, 31. C Evans, 35. Cleverley, 40. Amos, 42. Eikrem, 44. Dudgeon, 45. Gill.

No comments:

Powered By Blogger