Monday 16 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

LIGI KUU ENGLAND: Mechi za kwanza kwa kila Timu kwisha Jumatatu!
• Ni OLD TRAFFORD: Man United v Newcastle United!
Jumatatu, Agosti 16 usiku saa 4, saa za bongo, Manchester United itatinga Uwanja wa nyumbani Old Trafford kuikaribisha Timu mpya Ligi Kuu, Newcastle, walioshushwa Daraja Msimu wa 2008/9 lakini wakaibuka tena Ligi Kuu baada ya Msimu mmoja tu Daraja la chini.
Timu hizi zilipambana katika mechi ya ufunguzi ya Ligi Kuu Msimu wa 2008/9 kama hii ya kesho Uwanjani Old Trafford na kutoka sare 1-1.
Man United huenda ikamkosa Patrice Evra ambae ana maumivu kidogo ya mguu na ni wazi itawakosa Anderson, Ferdinand na Hargreaves ambao wote hawajapona maumivu yao.
Newcastle ina mlolongo wa majeruhi ambao ni Sol Campbell, Smith, Simpson, S Taylor, Gosling, na Best.
Vikosi vinategemewa:
Man United: Van der Sar, O’Shea, Vidic, Evans, Evra, Valencia, Carrick, Scholes, Giggs, Rooney, Nani
Akiba: Kuszczak, Brown, Rafael, Gibson, Obertan, Fabio, Park, Neville, Hernández, Smalling, Bébé, Fletcher, Owen, Berbatov, C Evans, De Laet
Newcastle: Harper, Williamson, Coloccini, Taylor, Enrique, Smith, Barton, Gutierrez, Carroll, Lovenkrands, Nolan.
Akiba: Forster, Krul, Campbell, Routledge, Perch, Xisco, Ameobi, Guthrie, Kadar, Ranger
Refa: C Foy.

No comments:

Powered By Blogger