Monday 16 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

UEFA yataja Majina 12 ya Wagombea Uchezaji Bora Ulaya
• Rooney ndie Mchezaji pekee LIGI KUU!!!
UEFA imetaja majina ya Wachezaji 12 watakaogombea Tuzo za Wachezaji Bora katika pozisheni na pia Mchezaji Bora wa Ulaya wa Mwaka.
Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa Alhamisi Agosti 26 kwenye Droo ya UEFA CHAMPIONS LIGI ya kupanga Makundi.
Wagombea waliotajwa wanagombea Uchezaji Bora kwenye pozisheni za Kipa, Beki, Kiungo na Fowadi.
Pia, Mchezaji mmoja atachaguliwa kuwa ndie Mchezaji Bora Ulaya wa Mwaka.
Wachezaji hao Bora watachaguliwa na Makocha wa Timu 16 zilizocheza hatua ya Mtoano ya Msimu uliopita wa 2009/10 wa UEFA CHAMPIONS LIGI.
Listi ya Wagombea:
• KIPA BORA:
Júlio César (FC Internazionale Milano)
Hugo Lloris (Olympique Lyonnais)
Víctor Valdés (FC Barcelona)
• BEKI BORA:
Lúcio (FC Internazionale Milano)
Maicon (FC Internazionale Milano)
Gerard Piqué (FC Barcelona)
• KIUNGO BORA:
Xavi Hernández (FC Barcelona)
Arjen Robben (FC Bayern München)
Wesley Sneijder (FC Internazionale Milano)
• FOWADI BORA:
Lionel Messi (FC Barcelona)
Diego Milito (FC Internazionale Milano)
Wayne Rooney (Manchester United FC)

No comments:

Powered By Blogger