Friday 20 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Cole ataka radhi kwa kukosa Penalti
Joe Cole amebeba lawama zote kwa kukosa kufunga penalti katika mechi ya jana ya EUROPA LIGI dhidi ya Trabzonspor ya Uturuki ambayo Liverpool walishinda 1-0.
Goli la Liverpool lilifungwa na Ryan Babel baada ya pande la Joe Cole.
Cole ametamka: “Ni bahati mbaya lakini ilikuwa penalti mbovu! Sijawahi kupiga penalti Miaka 15 sasa na itabidi ningoje Miaka 15 ili nipige nyingine!”
Mpiga penalti wa kawaida wa Liverpool kawaida ni Nahodha wao Steven Gerrard lakini jana alipumzishwa.
Kwa Joe Cole, hiyo ni mechi yake ya pili kuichezea Klabu yake mpya Liverpool na katika mechi ya kwanza walipotoka sare 1-1 na Arsenal Jumapili iliyopita alitwangwa Kadi Nyekundu.
Alhamisi ijayo Liverpool itakwenda Uturuki kurudiana na Trabzonspor.

No comments:

Powered By Blogger