Saturday 21 August 2010

PAULO ZE PWEZA: Aunga mkono Nchi yake England!!
Ingawa imeelezwa amestaafu kutabiri matokeo ya mechi za Soka baada kujijengea Usupastaa alipokuwa akitabiri kwa usahihi wakati wa Fainali za Kombe la Dunia zilizochezwa huko Afrika Kusini, Pweza Paulo ameibuka na kuiunga mkono Nchi yake aliyozaliwa England kuwa ndio itashinda kinyang’anyiro cha kuwa Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 ambazo England ni mmoja wa Wagombea.
Paulo Ze Pweza kwa sasa anaishi kwenye bwawa lake kwenye Kituo cha Viumbe wa Baharini kiitwacho Sea Life huko Oberhausen, Ujerumani lakini alizaliwa huko Weymouth, England Mwaka 2008.

No comments:

Powered By Blogger