Thursday 24 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Bia zawatia stimu England!!
Wachezaji wa England waliruhusiwa kunywa bia katika mkesha wa Siku ambayo walitakiwa kucheza mechi muhimu na Slovenia ambayo ilibidi washinde ili kusonga mbele Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia.
Hilo limethibitishwa na Kocha wa England, Fabio Capello, ambae alisema: “Tuliwaruhusu wanywe Bia. Na kweli siku ya pili Timu ilibadilika na ile ari yao ya zamani ilirudi tena! Walicheza vizuri na kujituma sana kupita mechi za USA na Algeria!”
England iliifunga Slovenia 1-0 na kutinga Raundi ya Pili kucheza na Germany Jumapili Juni 27

No comments:

Powered By Blogger