Tuesday 22 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Ni Argentina v Mexico & Uruguay v South Korea Raundi ya Pili!
-Nigeria NJE!!!
Katika mechi za leo Jumanne Juni 22, Argentina na Korea Korea Kusini zimetinga Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia na Argentina watacheza na Mexico na Korea Kusini wataivaa Uruguay katika Raundi hiyo.
Argentina waliibwaga Ugiriki kwa bao 2-0 kwa bao za Kipindi cha Pili zilizofungwa na Demichelis na Palermo.
South Korea walitoka sare na Nigeria ya goli 2-2.
Mabao ya Nigeria yamefungwa na Uche na Yakubu, kwa penalti.
South Korea walipata bao zao toka kwa Lii Jung-Soo na Park Chu-Young.
Kwa Afrika, Nigeria imeungana na Wenyeji Afrika Kusini na Cameroun kuwa nje ya Kombe la Dunia na kuwabakisha Ghana, Algeria na Ivory Coast huku Ghana ikiwa pekee ndio yenye nafasi kubwa kuingia Raundi inayofuata.

No comments:

Powered By Blogger