Friday 25 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Cannavaro akiri Italia vijeba!!
Fabio Cannavaro amewataka Viongozi Italy wawekeze katika kuwaendeleza Vijana baada ya Timu yao iliyonyakua Kombe la Dunia Mwaka 2006 kutolewa Raundi ya Kwanza tu ya Kombe la Dunia huko Afrika Kusini kwa kumaliza Kundi lao kwa kupigwa 3-2 na Slovakia hivyo kubaki mkiani huku Timu ‘vibonde’ New Zealand ikiwa juu yao.
Cannavaro, Miaka 36, aliekuwa Nahodha wa Italy na anaejiuzulu kuchezea Timu ya Taifa, amekiri: “Lazima tuendeleze Vijana! Lazima tujifunze toka aibu hii la sivyo itachukua tena Miaka 27 kushinda tena Kombe la Dunia.”
Timu ya Italy iliyocheza huko Afrika Kusini ilikuwa na Wachezaji 9 wenye umri zaidi ya Miaka 30.
Kustaafu kwa Cannavaro kunamfanya Kipa Gianluigi Buffon awe ndio Kepteni mpya wa Italy.
Pia Cannavaro anaenda Dubai kuchezea Klabu yake mpya Al-Ahli ya huko.
Italia itakuwa na Kocha mpya Cesare Prandelli kuanzia Julai 1.

No comments:

Powered By Blogger