Wednesday 23 June 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

KOMBE LA DUNIA:
Kimbembe cha Kesho cha kuingia Raundi ya 2
KUNDI E:
Msimamo:
-Holland pointi 6
-Japan pointi 3
-Denmark pointi 3
-Cameroun pointi 0
Mechi: Holland v Cameroun na Denmark v Japan
Holland tayari wako Raundi ya Pili na watajihakikishia kuwa vinara wa Kundi ikiwa hawatafungwa na Cameroun ambayo tayari ishaaga Kombe la Dunia.
Japan, wasipofungwa na Denmark, wataungana na Holland kusonga Raundi ya Pili.
Denmark lazima waifunge Japan ili watinge Raundi ijayo.
KUNDI F:
Msimamo:
-Paraguay pointi 4
-Italy pointi 2
-New Zealand pointi 2
-Slovakia pointi 1
Mechi: Slovakia v Italy na Paraguay v New Zealand
Kundi hili linahitaji mahesabu kidogo.
Paraguay wanahitaji sare tu dhidi ya New Zealand ili watinge Raundi ya Pili lakini New Zealand wakishinda wao ndio watasonga ingawa Paraguay wanaweza kusonga kutegemea na matokeo ya mechi nyingine ya Slovakia v Italy.
Italy lazima wawafunge Slovakia lakini sare inaweza kuwa sawa kwao ikiwa New Zealand watafungwa na Paraguay.
Ikiwa Slovakia wataifunga Italy wanaweza wakapenya ikiwa tu New Zealand wataifunga Paraguay na tofauti ya magoli itawasaidia.
Ni chemsha bongo hii!!

No comments:

Powered By Blogger