Friday 25 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Kanu ang’atuka Nigeria
Nahodha wa Nigeria, Kanu, ametangaza rasmi kujiuzulu kuichezea Timu ya Taifa ya Nigeria baada ya kuichezea kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini na kutolewa Raundi ya Kwanza.
Hata hivyo Kanu alidokeza kabla ya kushiriki Mashindano hayo atajiuzulu na alianza kuichezea Nigeria tangu Mwaka 1994 na kucheza mechi 80.
Kanu amewahi kushinda Kombe la Dunia kwa Vijana Chini ya Miaka 17, Medali ya Dhahabu ya Olimpiki na pia kumaliza wakiwa Washindi wa Pili na wa Tatu Kombe la Mataifa ya Afrika.
Kanu ameshawahi kuwa Mchezaji Bora Afrika mara mbili Mwaka 1996 na 1999.
Kanu amechezea Fainali za Kombe la Dunia mara tatu Mwaka 1998, 2002 na 2010.

No comments:

Powered By Blogger