Tuesday 22 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

KOMBE LA DUNIA:
RATIBA-Jumatano Juni 23
Saa 11 jioni: KUNDI C
Slovenia v England Nelson Mandela, Port Elizabeth
USA v Algeria Loftus Versfed, Pretoria
Saa 3.30 usiku: KUNDI D
Ghana v Germany Soccer City, Soweto, Johannesburg
Australia v Serbia Mbombela, Nelspruit
PATASHIKA YA KUINGIA RAUNDI YA PILI: Makundi C & D wacheza mechi za mwisho kesho Jumatano Juni 23
KUNDI C:
Msimamo:
-Slovenia pointi 4
-USA pointi 2
-England pointi 2
-Algeria pointi 1
Mechi: Slovenia v England na Algeria v USA
Slovenia wanahitaji sare na England ili wafuzu kuingia Raundi ya Pili lakini wanaweza pia kufuzu hata kama wakifungwa endapo USA na Algeria zitatoka sare.
England lazima washinde ili wasonge mbele.
Ikiwa England na USA watatoka sare katika mechi zao, tofauti ya magoli itahesabiwa ili kumpata Mshindi atakaeungana na Slovenia kutinga Raundi ya Pili na ikiwa hata magoli ni sawa basi itapigwa kura ili kuamua nani ataendelea.
Algeria watasonga mbele tu iwapo wataifunga USA kwa zaidi ya bao mbili.
Hakika ni hesabu kali mno.
KUNDI D:
Msimamo:
- Ghana pointi 4
-Germany pointi 3
-Serbia pointi 3
-Australia pointi 1
Mechi: Ghana v Germany na Serbia v Australia
Ghana na Ujerumani zitaingia Raundi ya Pili zikitoka sare kwenye mechi yao na Serbia wakitoka sare na Australia.
Ushindi kwa Ujerumani au Ghana na Serbia una maana Timu hizo zitasonga mbele.
Lakini Serbia wanaweza kufuzu hata wakitoka droo ikiwa tu Ujerumani itaifunga Ghana kwa zaidi ya bao moja au Ghana ikiifunga Ujerumani.
Australia wanahitaji waifunge Serbia ushindi mnono huku wakiomba mechi nyingine ya Ghana v Ujerumani inaisha sare au Timu moja inafungwa vibaya sana.
Haya ni mahesabu magumu mno.

No comments:

Powered By Blogger