Friday 25 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Spain, Chile zapita!!
Ni Brazil v Chile  & Spain v Ureno Raundi ya Pili!!
Spain imeifunga Chile bao 2-1 na kuingia Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia na pia ushindi huu umewafanya kuwakwepa Brazil Raundi ya Pili kwa kumaliza Kundi H wakiwa juu.
Spain watakutana na jirani zao Ureno na Brazil watacheza na wenzao toka Marekani ya Kusini Chile.
Mabao ya Spain yalifungwa na David Villa na Iniesta.
Rodrigo Millar ndie alieipa Chile bao.
Marco Estrada wa Chile alitolewa kwa Kadi Nyekundu na Refa Rodriguez toka Mexico kwa kosa la kutatanisha baada ya Fernando Torres kujidondosha wakati ilionekana wazi hakutegewa.
Uswisi 0 Honduras 0
Uswisi na Honduras zimetoka sare 0-0 katika mechi nyingine ya Kundi H na hivyo wote kutolewa nje ya Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger