Thursday 24 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

RAUNDI YA PILI: Germany v England!!
Ghana yafungwa, yatinga Raundi ya Pili!
Ghana imefungwa na Ujerumani bao 1-0 lakini imeitoa kimasomaso Afrika kwa kutinga Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia na itakutana na USA kwenye Raundi hiyo Jumamosi Juni 26.
Bao la Ujerumani lilifungwa kipindi cha pili na Mezut Ozil dakika ya 60.
Utamu mwingine wa pambano hili ni kwa Ndugu wawili kuwa Timu tofauti kwa Jerome Boateng kuichezea Ujerumani na Kevin-Prince Boateng kucheza Ghana, Nchi ambayo Baba yake alitoka.
Ujerumani itakutana na Watani zake wa Jadi, England, kwenye Raundi ya Pili.
Australia 2 Serbia 1
Australia wameitwanga Serbia bao 2-1 na kuhakikisha Nchi zote mbili zinarudi kwao mapema baada ya Ghana na Ujerumani kufuzu kwenye Kundi lao.
Mabao ya Australia yalifungwa na Tim Cahill, alierudi Uwanjani leo baada ya kukosa mechi moja kwa kutumia kifungo alipopewa Kadi Nyekundu ya uonevu katika mechi ya kwanza dhidi ya Ujerumani, na la pili na Holman.
Bao la Serbia alipachika Pantelic.
RAUNDI YA PILI: MTOANO TIMU 16 yaanza kukamilika!!
Jumamosi Juni 26
Saa 11 jioni:
URUGUAY v SOUTH KOREA
Nelson Mandela, Port Elizabeth
Saa 3.30 usiku:
USA v GHANA
Royal Bafokeng, Rustenburg
Jumapili Juni 27
Saa 11 jioni:
GERMANY v ENGLAND
Free State, Bloemfontein
Saa 3.30 usiku:
ARGENTINA v MEXICO
Soccer City, Soweto

No comments:

Powered By Blogger