Friday 25 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Japan yaingia Raundi ya Pili pamoja na Holland,  yaipiga Denmark 3-1
Holland imeifunga Cameroun bao 2-1 na kujihakikishia kuongoza Kundi E na hivyo kukutana na Slovakia hapo Jumatatu Juni 28 kwenye Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia.
Katika mechi hii Robin Van Persie alifunga bao la kwanza dakika ya 36 na Samuel Eto'o akasawazisha kwa Cameroun dakika ya 65 kwa penalti.
Huntelaar akafunga bao la pili kwa Uholanzi dakika ya 83 na kuwapa ushindi wao wa 3 kwenye Kundi lao.
Katika mechi nyingine, Japan ilichukua nafasi ya pili walipoifunga Denmark bao 3-1.
Japan watacheza na Paraguay Raundi ya Pili.
Magoli ya Japan yalufungwa na Honda dakika ya 17, Endo dakika ya 30 na Okazaki dakika ya 87.
Goli la Denmark alifunga Tomasson dakika ya 81.

No comments:

Powered By Blogger